"Usiku huu, naomba maombi yako kwa wote wanaohuzunika, kwa watoto ambao ulimwengu wao umevunjika, kwa wote ambao hisia zao za usalama zimefadhaishwa. Naomba wapate faraja kutoka kwa nguvu kubwa kuliko sisi wote, iliyotamkwa kupitia miaka katika Zaburi 23: "Hata nikitembea kati ya bonde la kivuli cha mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana Wewe u pamoja nami.", ni maneno ya kutia moyo yaliyosemwa na raisi wa 43 wa marekani George W Bush baada ya kutokea tukio tata la septemba 11, 2001.
Zaburi 23 ni moja kati ya zaburi maarufu inayojulikana na kukaririwa na watu wengi sana ikiwemo watoto. Imekuwa ikifundishwa kwa miaka mingi makanisani kama moja ya zaburi zenye kutia moyo na kuleta amani kwa anayepitia magumu au mambo mazito.
Nguvu ya Zaburi ya 23 ni uzoefu wa maisha ya uchungaji wa mfalme daudi akihusianisha na nguvu ya Mungu katika kuweza kuokoa na kubariki watu wote wanaomuamini.

